Dereva Daraja La II (x 4) Halmashauri ya Wilaya ya Hai

Application Deadline: 27 May 2015
Dereva Daraja La II (x 4) POSITION DESCRIPTION:
From Mwananchi

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WlLAYA YA HAl ANAWATANGAZIA WATANZANIA NAFASI ZA KAZI ZA UDEREVA KWA WENYE SIFA ZINAZOTAKIWA, KUOMBA KUJAZA NAFASI HIZO:-

MASHARTI YA UJUMLA KWA WAOMBAJI WOTE:
i.Awe Raia wa Tanzania na wenye umri miaka 18 usiozidi miaka 45
ii. Waombaji wote wambatishe cheti cha kuzaliwa
iii. Waombaji- waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed CV)
yenye anuani na namba ya simu za kuaminika na majina ya wadhamini - (Referees) watatu wa kuaminika. .
iv. Maombi yote yaambatane na vivuli vya vyeti vya taaluma, picha za 'Passport size' mbili, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa
wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa
kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe vizuri kuondoa
uwezeKano wa kudondoka au kupotea
v.Testmonials,provisional Results," statement of results" hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA
vi. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa
na kuidhinishwa narnamlaka husika (TCU NA NACTE)'
vii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za
kuingilia kutoka kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi
ya nafsi za kazi kwa wajiri wao.
viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba
isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu kiongozi.

Dereva Daraja La II (NAFASI 4)

MAJUKUMU YA KAZI
I Kuendesha magari ya aina zote ya Halmashauri
ii.Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri wakati wote, na kufanya uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji matengenezo
iii. Kufanya matengenezo madogomadogo katika gari
iv. Kutunza na kuandika daftari la safari Long-book kwa safari zote

SIFA ZA MWOMBAJI
Wenye cheti cha mtihani wa kidato cha nne, wenye leseni daraja C ya uendeshaji
pamoja na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua miaka mitatu bila
kusababisha ajali. Wenye cheti cha majaribio ya ufundi daraja la II (Trade test II)

MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaaani ngazi ya mshahara TGOS A kwa mwezi.
APPLICATION INSTRUCTIONS:
BARUA ZITUMWE KUPITIA POSTA KWA ANUANI IFUATAYO:- MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA
S.L. P 27,
HAl.
Simu Namba: 27-2758441
MAOMBI YATUMWE NDANI YA SIKU ISHIRINI NA MOJA (21)TANGU
KUTANGAZWA
Wale ambao wataitwa kwenye usaili watajulishwa siku na tarehe ya usaili.

KATIBU WA BODI YA AJlRA HALMASHAURI YA WlLAYA HAl
Dereva Daraja La II (x 4) Halmashauri ya Wilaya ya Hai Dereva Daraja La II (x 4)  Halmashauri ya Wilaya ya Hai Reviewed by ISSAH JUMA on Monday, May 11, 2015 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.