Mtendaji Wa Kijiji Daraja La III- (Nafasi 43) Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nanyumbu

Application deadline 2017-09-19
Location
Nanyumbu Mtwara
Description
Daily News 30/8/2017
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu anawatangazia Wananchi wote Raia wa Tanzania kuomba kujaza nafasi zifuatazo
MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III- (NAFASI 43)
SIFA ZA MWOMBAJI
Muombaji anatakiwa awe na Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya cheti (Astashahada) katika moja ya fani zifuatazo:- .
Utawala, Sheria, Elimu ya jamii, Usimamizi wa fedha, Maendeleo ya jamii na sayansi ya sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au Chuo chochote kinachotambulika na Serikali.
MSHAHARA
Ngazi ya mshahara ni TGS B yaani ni Tshs 390,000/= hadi 489,000/= Kwa mwezi. Na utaanza na mshahara wa Tshs 390,000/=
KAZII MAJUKUMU VA MTENDAJI WA KIJIJIII
i. Afisa masuuli na Mtendaji wa Serikali za Kijiji.
ii. Kusimamia ulinzi na Utawala bora wa Raia na mali zao, kuwa mlinzi wa amani na usimamizi wa Utawala bora katika Kijiji.
iii. Kujibu na kusimamia upangaji na utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Kijiji.
iv. Katibu wa mikutano na Kamati zote za Halmashauri ya Kijiji.
v. Kutafsiri na kusimamia Sera, na Taratibu.
vi. Kuandaa taarifa za utekelezaji na kazi katika eneo lake na kuhamasisha uchumi katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa umasikini na kuongeza uzalishaji mali.
vii. Kiongozi na Mkuu wa Idara na Vitengo vya Kitaaluma katika Kijiji.
viii. Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka za Kijiji.
ix. Kujibu na kuandaa taarifa za utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuziwasilisha kwenye Halmashauri ya kijiji na baadaye kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji na Kata.
x. Kiongoziwa Mkuu wa Vitengo vya Kitaaluma katika Kijiji.
xi. Kusimamia ukusanyaji wa kumbukumbu za malipo kodi, wataalamu mbalimbali na NGO zilizopo katika Kijiji.
NB: MAELEZO YA JUMLA.
i. Waombaji wenye sifa, taaluma na uwezo wa kuandika barua zao kwa mkono wambatanishe nakala zaVyetl vyao vya kuhitimu shule na mafunzo vyeti vinavyoonyesha kiwango cha kufahulu na siyo "Leaving Cectificate”
ii. Maelezo binafsi (CV) na nyaraka zote muhimu parnoja na picha (passport size 2) zilizopigwa karibuni.
iii. IIi kurahisisha mawasiliano waombaji wote wanasisitizwa kuonyesha namba zao za simu ya mezani, mkononi au fax namba chini yaanuanl yake.
iv. Waombaji ambao wapo katika ajira wanasisitizwa kupitisha barua zao za maombi kwa waajiri wao wasasa,
v. Waombaji wote wawe Rala wa Tanzania na wenye Umri kati ya miaka 18-45.

APPLICATION
Barua za maombi ziandikwe kwa mkono na ziambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, Taaluma na CV na maombi yote yatumwe kwa:-
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu
S. L. P 246
NANYUMBU
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 19/09/2017 saa 9:30
Mtendaji Wa Kijiji Daraja La III- (Nafasi 43) Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nanyumbu Mtendaji Wa Kijiji Daraja La III- (Nafasi 43) Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nanyumbu Reviewed by ISSAH JUMA on Tuesday, September 12, 2017 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.