Mtunza Kumbukumbu Msaidizi Chuo Cha Madini Mafuta na Gesi Shinyanga

    Application Deadline: 03 Jul 2015
     
    Mtunza Kumbukumbu Msaidizi POSITION DESCRIPTION: 1. Nafasi: Mtunza Kumbukumbu Msaidizi
    2. Idara: Utawala
    3. Kuripoti: Afisa Tawala

    Sifa:
    1. Checti au diploma katika elimu ya kutunza kumbukumbu au inayofanana na hiyo
    2. Ajue dhana ya utunzaji wa kumbukumbu
    3. Ajue kuwasiliana vizuri
    4. Awe na ufahamu wa kompyuta na hasa database
    5. Awe na rekodi nzuri ya kutunza siri kwa taarifa za kiofisi
    6. Awe na uwezo wa kufanya kazi nyingi peke yake na kwa muda uliotakiwa
    7. Awe na uwezo wa kufanya kazi masaa mengi
    8. Ajue kuwahudumia wateja
    9. Mtu anayependa kazi yake, kujiendeleza zaidi kupitia kusoma vitabu na masomo ya darasani

    Kazi zake
    1. Kutunza kumbukumbu za chuo
    2. Atahakikisha kuwa kumbukumbu zote zimekusanywa, zimefanyiwa kazi, zimehifadhiwa na kulindwa
    3. Kutunza, kulinda na kudumisha usiri wa taarifa za chuo kulingana na sera za Utunzaji wa Kumbukumbu na Utoaji wa taarifa za chuo kwenye uma.
    4. Kuwezesha wadau kupata mafaili yaliyotunzwa kwa kufuata itifaki husika.
    5. Kuanzisha, kufanya upya na kusimamia utunzaji wa kumbukumbu katika kituo kimoja.
    6. Kuanzisha na kusimamia mfumo wa kufuatilia mafaili
    7. Kutunza na Kusimamia rikodi zote ikiwa ni pamoja na barua, emails na kuziingiza na kuzitoa kwa mfumo mzuri.
    8. Atasaidia kuwafundisha watumiaji wa ndani juu ya utunzaji salama wa kumbukumbu na mifumo yake.
    9. Atasaidi katika kubuni, kutekeleza na kuhakiki sera za utunzaji wa kumbukumbu za chuo ili ziendane na sera za nchizinazohusiana na taarifa.
    10. Ataandaa na kutuma kwa msimamizi wake ripoti za utunzaji wa kumbukumbu kwa wiki na mwezi
    11. Atafanya kazi zingine kama atakavyoagizwa na msimamizi wake
     
    APPLICATION INSTRUCTIONS: Tuma barua yako ya maombi na CV kwa:
    Mkuu wa Chuo
    Chuo cha Madini Shinyanga
    Ndala, Shinyanga: Plot No. 91, Block HH
    SLP 1016, Shinyanga
Mtunza Kumbukumbu Msaidizi Chuo Cha Madini Mafuta na Gesi Shinyanga Mtunza Kumbukumbu Msaidizi Chuo Cha Madini Mafuta na Gesi Shinyanga Reviewed by ISSAH JUMA on Monday, June 08, 2015 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.